Artwork

Contenido proporcionado por Iran.Tanzania. Todo el contenido del podcast, incluidos episodios, gráficos y descripciones de podcast, lo carga y proporciona directamente Iran.Tanzania o su socio de plataforma de podcast. Si cree que alguien está utilizando su trabajo protegido por derechos de autor sin su permiso, puede seguir el proceso descrito aquí https://es.player.fm/legal.
Player FM : aplicación de podcast
¡Desconecta con la aplicación Player FM !

Mwanamalenga wa Kiirani Nezami

12:36
 
Compartir
 

Manage episode 337502594 series 3382153
Contenido proporcionado por Iran.Tanzania. Todo el contenido del podcast, incluidos episodios, gráficos y descripciones de podcast, lo carga y proporciona directamente Iran.Tanzania o su socio de plataforma de podcast. Si cree que alguien está utilizando su trabajo protegido por derechos de autor sin su permiso, puede seguir el proceso descrito aquí https://es.player.fm/legal.

Jamaluddin Abu Mohammad hakuweza kupata upendo wa wazazi wake kwa muda mrefu; kwani wazazi wake walifariki dunia akiwa bado mtoto na kupata malezi akiwa mtoto yatima. Ushahidi wa kihistoria unaonyesha kuwa, Nezami Ganjavi hakuwahi kuondoka katika mji wa Ganja akiwa bado na umri mdogo, na alipofikia marika ya ujana , aliweza kujifunza sanaa na ujuzi mbalimbali na hatimaye alikuwa na ufasaha wa kuzungumza na kuandika lugha za Kiazeri, Kiarabu, Kiajemi na Kipahlavi.

Nezami ni bingwa na mshairi anayepaswa kuzingatiwa kwenye mihimili na nguzo za ushairi wa Kiajemi. Yeye ni mmoja wa malenga aliyekuwa na kipaji cha kuandika mashairi na kuyasoma kwa sauti nzuri, iliyowavutia wasikilizaji. Ingawa hekaya na simulizi za hadithi za Kiajemi hazikuanzishwa na Nezami, lakini gwiji huyo anahesabiwa kuwa ni mshairi pekee aliyeweza kuendeleza ushairi wa mafumbo kwa kiwango cha juu zaidi kufikia mwisho wa karne ya sita.

Nezami aliweza kujiwekea nafasi maalumu katika fasihi ya lugha ya Kifarsi inayotumika Iran na ametumia takriban miaka thelathini ya maisha yake akitunga mkusanyiko wake wa mashairi yanayoitwa "Hazina Tano" au "Khamseh". Mkusanyiko huu una mashairi matano marefu, ambayo ni: "Makhzan al-Asrar", "Khosrow na Shirin", "Lalya na Majnoon", "Haft Peykar" na "Iskander Nameh" ni hazina tano. Pia, mkusanyo wa mashairi yaliyosalia kutoka kwa Nezami ni pamoja na mashairi, mashairi ya sauti vipande ambavyo vina nafasi maalumu katika fasihi ya Kiajemi.

Ingawa umaarufu mwingi wa Nezami unatokana na kutunga mashairi ya mapenzi, yenye hekima na sahili. Kwa maneno mengine, mashairi yake ni rahisi lakini ya kina, na mashairi yake yalikuwa yanamfanya mtu kufikiria na kutafakari kwa kina ili kupata siri iliyofichwa katika maneno yake. Kuna jumbe nyingi za kifalsafa ambazo zimeelezwa kwa kutumia maneno mepesi na fasaha, badala ya kutumia maneno magumu na mazito. Nyingi za beti zake za mashairi zilikuwa zikielezea maisha ya akhera, sanjari na kuyafurahia maisha mafupi ya ulimwenguni.

Kuna tofauti za maoni kuhusu kuzaliwa kwa baba wa mshairi Nezami Ganjavi, na baadhi ya vyanzo vinaeleza kuwa anatoka Tafresh au Farahan. Lakini Behrouz Thorotian (mtafiti wa fasihi, mwanasayansi na profesa mstaafu) anaeleza kuwa, mwanzo wa beti za mashairi ya Layla na Majnoon, zinaonyesha kuwa alikuwa na asili ya Kiajemi. Ameendelea kusema kuwa, ubeti wa 36 wa shairi la Leyla na Majnoon, unafichua kazi na nafasi ya mshairi ambaye alikuwa Dehqan yaani “mkulima” na kuitambulisha jamii yake kuwa ni Muajemi.

Kwa Wairani neno Dehqan "mkulima" linamaanisha mmiliki wa ardhi ya kilimo; malenga Ferdowsi naye katika beti zake amefafanua kuwa, tafsiri ya neno hilo lilitumika baadaye kwa Wairani wote. Kwa kuongezea, neno Dehqan "mkulima" lilitumiwa pia kwa maana ya "mwanahistoria". Kwa hivyo, inaweza kueleweka kuwa Nezami Ganjavi anajitambulisha kama malenga, mkulima wa Iran, mwanahistoria, muimbaji wa mashairi na mmiliki wa ardhi ya kilimo. Wakulima wamekuwa na jukumu la kuhifadhi tamaduni na historia ya Iran katika kipindi cha Kiislamu, na kwa ufupi, familia ya Nezami Ganjavi inaweza kuchukuliwa kuwa familia ya wakulima wenye ufahamu wa kitamaduni na utajiri wa mali ambao wamekuwa na nafasi muhimu katika fasihi.

Nezami Ganjavi alikuwa mshairi mashuhuri, mwandishi wa riwaya, mwenye hekima na ambaye amekuwa na ushawishi mkubwa katika fasihi ya Kiajemi na daima ametajwa kuwa mtu muhimu katika historia.

Dola la Uajemi ni moja kati ya madola makubwa yaliyokuwa yakitawala duniani. Jamhuri ya Azerbaijan, iliyoko katika eneo la Caucasia kati ya Ulaya na Asia ilikuwa chini ya himaya ya dola la Uajemi katika zama hizo.

--- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message

  continue reading

12 episodios

Artwork
iconCompartir
 
Manage episode 337502594 series 3382153
Contenido proporcionado por Iran.Tanzania. Todo el contenido del podcast, incluidos episodios, gráficos y descripciones de podcast, lo carga y proporciona directamente Iran.Tanzania o su socio de plataforma de podcast. Si cree que alguien está utilizando su trabajo protegido por derechos de autor sin su permiso, puede seguir el proceso descrito aquí https://es.player.fm/legal.

Jamaluddin Abu Mohammad hakuweza kupata upendo wa wazazi wake kwa muda mrefu; kwani wazazi wake walifariki dunia akiwa bado mtoto na kupata malezi akiwa mtoto yatima. Ushahidi wa kihistoria unaonyesha kuwa, Nezami Ganjavi hakuwahi kuondoka katika mji wa Ganja akiwa bado na umri mdogo, na alipofikia marika ya ujana , aliweza kujifunza sanaa na ujuzi mbalimbali na hatimaye alikuwa na ufasaha wa kuzungumza na kuandika lugha za Kiazeri, Kiarabu, Kiajemi na Kipahlavi.

Nezami ni bingwa na mshairi anayepaswa kuzingatiwa kwenye mihimili na nguzo za ushairi wa Kiajemi. Yeye ni mmoja wa malenga aliyekuwa na kipaji cha kuandika mashairi na kuyasoma kwa sauti nzuri, iliyowavutia wasikilizaji. Ingawa hekaya na simulizi za hadithi za Kiajemi hazikuanzishwa na Nezami, lakini gwiji huyo anahesabiwa kuwa ni mshairi pekee aliyeweza kuendeleza ushairi wa mafumbo kwa kiwango cha juu zaidi kufikia mwisho wa karne ya sita.

Nezami aliweza kujiwekea nafasi maalumu katika fasihi ya lugha ya Kifarsi inayotumika Iran na ametumia takriban miaka thelathini ya maisha yake akitunga mkusanyiko wake wa mashairi yanayoitwa "Hazina Tano" au "Khamseh". Mkusanyiko huu una mashairi matano marefu, ambayo ni: "Makhzan al-Asrar", "Khosrow na Shirin", "Lalya na Majnoon", "Haft Peykar" na "Iskander Nameh" ni hazina tano. Pia, mkusanyo wa mashairi yaliyosalia kutoka kwa Nezami ni pamoja na mashairi, mashairi ya sauti vipande ambavyo vina nafasi maalumu katika fasihi ya Kiajemi.

Ingawa umaarufu mwingi wa Nezami unatokana na kutunga mashairi ya mapenzi, yenye hekima na sahili. Kwa maneno mengine, mashairi yake ni rahisi lakini ya kina, na mashairi yake yalikuwa yanamfanya mtu kufikiria na kutafakari kwa kina ili kupata siri iliyofichwa katika maneno yake. Kuna jumbe nyingi za kifalsafa ambazo zimeelezwa kwa kutumia maneno mepesi na fasaha, badala ya kutumia maneno magumu na mazito. Nyingi za beti zake za mashairi zilikuwa zikielezea maisha ya akhera, sanjari na kuyafurahia maisha mafupi ya ulimwenguni.

Kuna tofauti za maoni kuhusu kuzaliwa kwa baba wa mshairi Nezami Ganjavi, na baadhi ya vyanzo vinaeleza kuwa anatoka Tafresh au Farahan. Lakini Behrouz Thorotian (mtafiti wa fasihi, mwanasayansi na profesa mstaafu) anaeleza kuwa, mwanzo wa beti za mashairi ya Layla na Majnoon, zinaonyesha kuwa alikuwa na asili ya Kiajemi. Ameendelea kusema kuwa, ubeti wa 36 wa shairi la Leyla na Majnoon, unafichua kazi na nafasi ya mshairi ambaye alikuwa Dehqan yaani “mkulima” na kuitambulisha jamii yake kuwa ni Muajemi.

Kwa Wairani neno Dehqan "mkulima" linamaanisha mmiliki wa ardhi ya kilimo; malenga Ferdowsi naye katika beti zake amefafanua kuwa, tafsiri ya neno hilo lilitumika baadaye kwa Wairani wote. Kwa kuongezea, neno Dehqan "mkulima" lilitumiwa pia kwa maana ya "mwanahistoria". Kwa hivyo, inaweza kueleweka kuwa Nezami Ganjavi anajitambulisha kama malenga, mkulima wa Iran, mwanahistoria, muimbaji wa mashairi na mmiliki wa ardhi ya kilimo. Wakulima wamekuwa na jukumu la kuhifadhi tamaduni na historia ya Iran katika kipindi cha Kiislamu, na kwa ufupi, familia ya Nezami Ganjavi inaweza kuchukuliwa kuwa familia ya wakulima wenye ufahamu wa kitamaduni na utajiri wa mali ambao wamekuwa na nafasi muhimu katika fasihi.

Nezami Ganjavi alikuwa mshairi mashuhuri, mwandishi wa riwaya, mwenye hekima na ambaye amekuwa na ushawishi mkubwa katika fasihi ya Kiajemi na daima ametajwa kuwa mtu muhimu katika historia.

Dola la Uajemi ni moja kati ya madola makubwa yaliyokuwa yakitawala duniani. Jamhuri ya Azerbaijan, iliyoko katika eneo la Caucasia kati ya Ulaya na Asia ilikuwa chini ya himaya ya dola la Uajemi katika zama hizo.

--- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message

  continue reading

12 episodios

Todos los episodios

×
 
Loading …

Bienvenido a Player FM!

Player FM está escaneando la web en busca de podcasts de alta calidad para que los disfrutes en este momento. Es la mejor aplicación de podcast y funciona en Android, iPhone y la web. Regístrate para sincronizar suscripciones a través de dispositivos.

 

Guia de referencia rapida